MalemboFarm *Kilimo* Talk on Clubhouse

MalemboFarm *Kilimo* Talk Clubhouse
803 Members
Updated: Mar 17, 2024

Description

kwa miaka mingi, umuhimu wa kilimo endelevu katika kuondoa njaa na umaskini umekuwa mjadala kuntu ulioleta ubishani, ukinzani wa hoja na uliochagizwa. Kwa siku za hivi karibuni, ukweli kuwa;kilimo endelevu ni kitovu cha malengo ya maendeleo hapa Tanzania na kimataifa haukwepeki tena.

Njia za kufikia ukweli huo zinabishaniwa, na mijadala juu ya sera sahihi, teknolojia na uwekezaji .

Ni kwa muono huu, Malembo Farm(MF) inakuletea progamu ya mjadala kuhusu masuala haya hapa nchini na kwingineko duniani uitwao “MF; KILIMO TALK”,utakaokuwa ukiletwa kwako kila siku za wiki kuanzia saa kumi na Moja jioni. 5:00pm EAT

Katika mijadala ya kilimo hivi sasa juu ya maendeleo; mambo makuu sita yanaibuka katika mijadala hiyo. *MF Kilimo Talk* tunayaweka katika mafungu yafuatayo.

1. Biashara, ruzuku na kilimo.

2. Uanzishwaji wa GMO,s

3. Umuhimu wa masoko na kilimo biashara.

4. Umuhimu wa kujitegemea kwa chakula( "Uhuru wa chakula") na ikolojia ya kilimo.

5. Uwekezaji wa sekta binafsi na kutwaliwa kwa rasilimali.

6. Mabadiliko ya tabia nchi.

Kwa nafasi ya kipekee kabisa tunamulika nafasi ya Vijana, Wanawake na Wastaafu Watarajiwa katika masuala haya nyeti.

MF; Kilimo Talk inalenga kuibua mijadala kuhusu mambo haya muhimu na mengine kwa faida ya nchi yetu.

#TafakuriJadidiKwaMstakabaliWaTaifaLetu

Last 30 Records

Day Members Gain % Gain
March 17, 2024 803 0 0.0%
January 26, 2024 803 +2 +0.3%
December 13, 2023 801 +1 +0.2%
November 03, 2023 800 -1 -0.2%
October 04, 2023 801 +3 +0.4%
September 04, 2023 798 +3 +0.4%
August 07, 2023 795 +4 +0.6%

Charts

Some Club Members

More Clubs